Sensa ya kwanza Tanzania ilifanyika mwaka 1910. Sensa nne za Mwisho zilifanyika baada ya Uhuru, katika miaka ya 1967, 1978, 1988 na 2002. Kulingana na sensa ya mwisho iliyofanyika mwezi Agosti 2002, idadi ya watu nchini Tanzania ilikuwa 34,443,603.
Umoja wa Mataifa unailezea Sensa ya Watu na Makazi kama ni “Mchakato
mzima wa kukusanya, kuchambua, kutathmini na kuchapisha au kusambaza
takwimu za kidemografia, kiuchumi na kijamii za watu wote nchini kwa
muda maalumu”
2. Sensa hufanyika wakati gani?
Sensa ya watu na makazi hufanyika kila baada ya miaka 10. Sensa ya 2012 itakuwa ni Sensa ya tano tangu kupatikana Uhuru.
3. Kwa nini sensa ni muhimu?
Madhumuni
ya kufanya sensa ni kuhakikisha upatikanaji wa takwimu muhimu na kwa
wakati kuhusiana na idadi ya watu nchini, kwa ajili ya matumizi katika
maandalizi ya sera, usimamizi, utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini ya
mafanikio ya programu mbalimbali za maendeleo nchini.
4. Sensa itaendeshwa kwa taratibu zipi za kisheria.
Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 itafanyika kulingana na Sheria ya Takwimu Namba 1 ya mwaka 2002.
5. Madhumuni hasa ya sensa ni yapi?
Madhumuni
ya kufanya sensa ni kuhakikisha upatikanaji wa takwimu muhimu na kwa
wakati kuhusiana na idadi ya watu nchini, kwa ajili ya matumizi katika
maandalizi ya sera, usimamizi, utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini ya
mafanikio ya programu mbalimbali za maendeleo nchini
http://www.nbs.go.tz/sensa2012/
No comments:
Post a Comment